UGANDA: Mwanamuziki Bobi Wine aachiwa kwa dhamana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mahakama moja mashariki mwa Uganda imemshtaki mgombea urais wa chama cha upinzani Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, kwa makosa ya kutenda kitendo chenye uwezekano wa kusambaza ugonjwa wa kuambukiza.



Bobi Wine alikamatwa katika mkutano wa kampeni Jumatano akishtumiwa kwa kukiuka miongozo ya kudhibiti ugonjwa wa virusi vya corona kwenye mkusanyiko wa hadhara.

Hata hivyo Bobi Wine amepewa dhamana.

Wakati huohuo, jeshi la Uganda limeongeza wanajeshi wake katika mji wa Kampala na miji mingine kukabiliana na maandamano yanayoendelea kuibuka.

Hadi kufikia sasa watu 28 wamethibitishwa kufariki dunia kote nchini humo wakati wa maandamano yaliyokuwa yakidai kuachiliwa huru kwa Bobi Wine huku wengine zaidi ya 500 wakikamatwa, kulingana na jeshi la polisi.

Maandamano hayo ya kudai kuachiliwa huru kwa Bobi Wine, yalisambaratishwa kwa kutumia vitoza machozi na wakati mwingine risasi zilitumiwa.

Awali, naibu msemaji wa jeshi, Kanali Deo Akiiki aliviambia vyombo vya habari kuwa wanajeshi watapelekwa katika barabara zote kuu zinazoingia mjini.

Januari 2021, Uganda itakuwa na uchaguzi mkuu wa urais lakini wiki za kwanza za kampeni tayari zimekubwa na vurugu na ghasia.

L
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad