Wabadhirifu fedha za umma kukiona -waziri Mpango

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Philip Mpango ameahidi kusimamia kikamilifu ubadhirifu wa fedha za umma huku akiwaonya watu wazembe na kuwataka wawapishe mapema .

Akizungumza mara baada ya kuapishwa katika ofisi za Ikulu mkoani Dodoma Dkt.Mpango amemshukuru Rais Magufuli kwa kumteua kwa mara nyingine tena kuendelea kuwa Waziri wa Fedha na Mipango huku akiwashukuru watanzania wote.


“Uzembe, wizi na ubadhirifu wa fedha za umma hilo nitalitilia kipaumbele cha juu bado naona shida kwenye miradi ya maendeleo bado tunaibiwa  kuna shida nitasimamia ili tuokoe fedha za hawa wanyonge zifanye kazi yake  na hao wazembe kwa kuwa umenipa kisu watupishe mapema kwa sababu mzigo huu ni mkubwa sana kazi hii ni gunia la misumari kwa hiyo watupishe.” Alisema Dkt. Mpango


Aidha Dkt.Mpango ameongeza kuwa  upo uwezekano katika kipindi kifupi na chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tanzania itakuwa nchi yenye hadhi ya kipato cha kati kwa kiwango cha juu.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad