Aongezewa urefu wa mwili kwa kuhofia kumkosa mke

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Kila mwaka mamia ya watu kote duniani hufanya upasuaji wa miguu ili waongezewe urefu wa kima chao cha mwili.Sam Becker mkazi wa jiji la New York nchini Marekani mwenye umri wa miaka 30 ni mmoja wa watu hao.



Anasema alipokuwa shule ya msingi alikuwa anaonekana kuwa mrefu kuliko wanafunzi wenzake, lakini la kushangaza alipomaliza shule ya sekondari alijipata yeye ndiye mfupi kuliko wenzake.



"Nilipoingia chuo kikuu nilijipata mimi ndiye mfupi kuliko vijana wote na hata wasichana’’ aalisema.



"Kusema ukweli hii iliniathiri sana maishani mwangu. Nikisema ukweli, wasichana hawakuwa wanataka kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wavulana wanaowazidi urefu wa kimo. Lakini jambo kubwa lililokuwa likinisumba akilini ni kufikiria kwamba huenda nisipate mke kwasababu ya ufupi wangu".



Baada ya kuzungumza na mama yake na kukubali athari anazoweza kuzipata, Sam alimua kuchukua uamuazi wa kufanyiwa upasuaji wa kuongeza urefu. Anasema mwaka 2015 upasuaji huo wa miguu yake yote miwili ulifanikiwa akaongezewa urefu kutoka sentimita 162 (162cm) hadi sentimita 170 (170cm).



Upasuaji wa kuongeza urefu wa kimo cha mwili huchukua muda mrefu na unaumiza. Na wataalamu wa afya wanasema upasuaji huu unaweza kuwa na madhara mabaya ya kiafya na muda mrefu.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad