“Ghasia zikitokea Trump atawajibika” Afisa Uchaguzi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Afisa Uchaguzi wa jimbo la Georgia nchini Marekani, Gabriel Sterling ameonya kuwa Rais Donald Trump atachukua jukumu la ghasia zozote zitakazojitokeza kutokana na madai ya udanganyifu katika uchaguzi ambayo hana uthibitisho


Katika taarifa yake, Sterling, kutoka Republican, amesema ni muda kwa Trump kuachana na hayo mambo.


“Kila kitu kimeenda mbali sana! Yani kila kitu! Inabidi kuachana na haya mambo!”


Jimbo la Georgia limefanya marudio ya kuhesabu kura kwa mara ya pili baada ya kampeni ya Trump kuomba kura zirudiwe kuhesabiwa.


Rais mteule wa Marekani, Joe Biden kutoka chama cha Democratic alitangazwa kuwa na ushindi mdogo katika jimbo hilo.


Msemaji wa kampeni za Trump, Tim Murtaugh amesema anajaribu kuhakiki kuwa kura zote zilihesabiwa na hakuna kura zilizoibiwa.


“Mtu yeyote asijihusishe katika vitisho na ghasia, na kama zimetokea tunalaani vikali vitendo hivyo,”


Akizungumza kwa ghadhabu katika mkutano na waandishi wa habari huko Atlanta jana Sterling, msimamizi wa mfumo wa upigaji kura aliwakemea wanachama wenzake wa Republicans, pamoja na rais.


Amesema, kwa miaka 20 ambayo amekuwa akisimamia mfumo wa upigaji kura katika uchaguzi wa taifa hilo, nadharia ya kutokubalika kwa ushindi, kumesababisha apate vitisho vya kuuawa na familia za wafanyakazi wamekuwa wakisumbuliwa, ameongeza.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mhhhhh....Mbona Makubwa !!! Mpaka Malekani Sanaa Mtindo Umoja.

    Si bola na yeye aende kule wanapo endaga


    ubeli Giji

    ReplyDelete

Top Post Ad