Kimewaka...Halima Mdee, Bulaya na Kishoa wabadili Wakili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Wabunge wa viti maalumu (Chadema), Halima Mdee, Ester Bulaya na Jesca Kishoa, wamemtambulisha wakili mpya atakayewatetea katika kesi yao ya mashtaka saba likiwemo la kufanya mkusanyiko na kutotii amri halali katika gereza la Segerea Jijini Dar es Salaam.

 

Wabunge hao ambao hivi karibuni walitangazwa kuvuliwa uanachama na Kamati Kuu ya Chadema leo Desemba 3, 2020 wamefika katika Mahakama ya Hakimu Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kesi ya kusomewa maelezo ya awali, wamewakilishwa na wakili Emmanuel Vkandis


Wabunge hao wanashtakiwa Mahakamani hapo na wenzao 24 ambao wote kwa pamoja hapo awali washtakiwa hao wote walikuwa wakitetewa na wakili Hekima Mwasipo.


Hata hivyo Mahakama imeshindwa kuwasomea washtakiwa hao kusomewa maelezo yao ya awali na badala yake imetoa hati ya kukamatwa kwa washitakiwa wawili, Edgar Adelini, Reginald Masawe, ambao hawajafika Mahakamani hapo leo bila taarifa yoyote. 


Mapema wakili wa serikali Ester Martin alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, kuwa kesi hiyo leo imeitwa kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo ya awali lakini washtakiwa wawili hawajafika hivyo wameomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuwasomea maelezo hayo na pia wameomba hati ya kukamatwa kwa washtakiwa hao.


Kati ya mashtaka hayo saba yanayowakabili, matatu ni ya kutoa lugha ya kuudhi yanayowakabili, Mdee, Bulaya na Jacob, moja ni kuharibu Mali, kufanya mkusanyiko usio kuwa wa halali, kutotii amri halali iliyowekwa na Jeshi la Magereza na shambulio.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad