Mwigizaji Taraji P. Henson Afunguka Kutaka Kujia Kipindi cha Janga la Corona

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Tatizo la afya ya akili (mental health) sio la kuchukulia poa hata kidogo, mwigizaji Taraji P. Henson amefunguka kwamba alipata mawazo ya kujiua kipindi ambacho alikuwa amejitenga peke yake kwa hofu ya ugonjwa wa Corona.


Kupitia kipindi chake 'Peace of Mind With Taraji' jana Jumatano kupitia ukurasa wake wa Facebook, mwigizaji huyo maarufu alikiri kufikia maamuzi hayo ya kutaka kujitoa uhai wake kutokana na upweke.

-

"Katika kipindi hiki cha janga la Corona imekuwa wakati mgumu sana kwetu sote, na nilipatwa na nyakati za giza. Nilikuwa kwenye eneo lenye kiza kinene, kwa siku kadhaa, sikuweza kunyanyuka kitandani, kitu ambacho kilinifanya kujiona kama sio mimi. Kisha nikaanza kupata fikra za kujimaliza, ilinitokea nyakati mbili za usiku mfululizo." alisema Taraji.


Baada ya fikra hizo alifikia uamuzi wa kununua bastola, na baadaye alianza kumuwaza mtoto wake wa Kiume ataishi vipi? lakini alijiambia kwamba "atasahau tu kwa sababu tayari ni kijana mkubwa." Kilichomsaidia Taraji. P. Henson ni uamuzi wake wa kuanza kuongea na wapendwa wake na kutoa ya moyoni kiasi ambacho ilimsaidia kutokaa na kitu moyoni na kupunguza msukumo wa moyo wake.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad