Nawaomba kwa heshima kubwa mtuheshimu ndio tuwaheshimu', Uhuru Kenyatta

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

'

Rais Uhuru Kenyatta hii leo amefungua rasmi kongamano la magavana kujadili mikakati ya kuboresha uchumi jijini Nairobi.


Katika hotuba yake, Rais Uhuru Kenyatta ametupia kidole cha lawama nchi za nje juu ya kile alichosema ni kujaribu kuingilia na kuelekeza Kenya namna ya kuendesha shughuli zake.



Kiongozi huyo wa nchi amesema, Kenya inashukuru uungwaji mkono na ushirikiano inayopata kutoka kwa nchi zingine lakini nchi yake haitakubali kulazimishwa cha kufanya na yeyote yule.



“Tunashukuru maafisa wa Umoja wa Mataifa na washirika wengine wa maendeleo ambao wamekuwa karibu sana lakini hadi kufikia sasa lazima niweke wazi, wakati tunawashukuru kwa ushirikiano wenu na kutajarajia ushirikiano zaidi, lazima mkumbuke Kenya ina wenyewe na wenyewe ni Wakenya milioni 50,” amesema Kenyatta.



Aidha, Rais Uhuru Kenyatta aliwaomba kujizuia kujaribu kuwaelekeza cha kufanya na njia ya kufuata.



“Tunakoelekea kuko wazi. Tunakuomba ujiunge nasi, utuunge mkono katika juhudi zetu hizo. Lakini usiingilie kwasababu hatutakuruhusu uamuru njia tunayostahili kufuata. Nawaomba kwa heshima kubwa mtuheshimu ndipo tutakapo waheshimu. Kila mtu yuko na shida zake hata wao wana shida zao wanazohitajika kuzitatua huko kwao. Nasema hivyo kwa nia njema tu. Sitaruhusu hilo na kama nchi hatutaruhusu hilo.”


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. My Dear Bro Uhuru Mwigai Kenyatta, Hivi ndivyo tunavyotaka
    ita a well said, perfectly worded kwamba sisi tunajitambua hapa na tuna maamuzi yetu tunayo yataka kwa faida yetu.

    Nimemsikiia Pia Paul Kagame akiwaonya nchi za Ulaya.

    WE NEED A STRONG AFRIKA WITH SIMILAR VOICE AND GOAL.

    ReplyDelete

Top Post Ad