Robert Lewandowski ashinda tuzo ya mwanasoka bora wa Fifa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Robert Lewandowski , msahambuliaji nyota wa Bayern Munich alishinda tuzo ya mwanasoka bora wa Fifa huko Zurich na kuwashinda washindi wa miaka iliyotangulia ,Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

Mshambuliaji huyo kutoka Poland alifunga mabao 55 katika michezo 47 tu msimu uliopita na kuisaidia miamba ya Ujerumani Bayern Munich kunyakua mataji 3 katika msimu moja,yaani kombe la ligi ya Ujerumani,kombe la taifa na ligi ya mabingwa ulaya.


Lewandowski mwenye umri wa miaka 32, alimaliza msimu akiwa mfungaji bora wa ligi, kombe la taifa na Ligi ya Mabingwa.


Mlinzi wa Manchester City Lucy Bronze alishinda tuzo ya mchezaji bora wa wanawake.


Washindi waliamuliwa na uteuzi kutoka kwa manahodha wa timu za mataifa na makocha wakuu, kura ya mtandaoni ya mashabiki na wawakilishi 200 wa vyombo vya habari.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad