Waandamanaji Wanaomuunga Mkono Trump Wazua Ghasia Katika Miji ya Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Maelfu ya wafuasi wa Rais Donald Trump wanaodai kulikuwa na wizi wa kura wamekutana katika miji tofauri ya Marekani mwishoni mwa Juma na kusababisha ghasia walipokabiliana na waandamanaji wanaompinga.

Mjini Washington DC, zaidi ya watu 20 walikamatwa na wengine wanne walichomwa visu, kulingana na polisi.


Bw Trump alishindwa katika uchaguzi wa tarehe 3 Novemba na Bw Joe Biden lakini bado hajakubali kushindwa.


Wajumbe ambao kulingana na mfumo wa Marekani ndio wanaomchagua rais wanakaribia kuidhinisha ushindi wa Bw Biden leo Jumatatu.


Bw Biden alichaguliwa kwa kura 306 na Trump 232 katika kura za wajumbe - Electoral College, na kupata zaidi ya kura milioni saba kuliko hasimu wake wa Republican katika kura za wananchi.


Katika mji mkuu wa Marekani, polisi waliwatenganisha waandamanaji kwa kuwaweka pande mbili, mkakati ambao ulihusisha kufungwa kwa mlango la Black Lives Matter Plaza ambako waandamanaji waliokuwa wakipinga hatua ya Trump kukataa kushindwa walikuwa wamekusanyika.


Waandamanaji wanaomuunga mkono Trump , wakiandamana chini ya kauli mbiu waliyoiandika kwenye mabango inayosema "acha kuiba ", waliungwa mkono na wajumbe wa kikundi cha mrengo wa kulia kinachojiita Proud Boys, waliokuwa wamevalia mavazi ya rangi za manjano na nyeusi, wengi wao wakiwa wamevalia fulana za kujikinga na risasi.


Bw Trump alisababisha utata kwa kusema kuwa kikundi hicho kinapaswa " kujitokeza na kuwa kuwa chonjo" wakati wa mdahalo wa uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi Desemba, ingawa baadaye alilaani "wanaharakati wote wanaotetea maslahi ya wazungu".


Kadri giza lilivyokuwa likiingia , waandamanaji wa Proud Boys na Antifa dhidi ya Trump , walikuwa wametenganishwa na polisi kwa kiasi kikubwa walikuwa wakirushiana matusi makali. Hatahivyo ghasia za hapa na pale ziliibukaa na kuzimwa na polisi.


Matukio ya kuchomana visu yalitokea karibu na baa ya Harry iliyopo katikati mwa Washington DC , lakini haikufahamika wazi waliodungwa visu walikuwa ni wa kundi gani, kuliongana na Gazeti la Washington Post.


Watu wanane walipelekwa hospitalini, wakiwemo maafisa wawili wa polisi , kulingana na televisheni ya CNN.


Waandamanaji wa kikundi cha Make America Great Again (MAGA) ,wanaomuunga mkono Bw Mr Trump, walinaswa kwenye kamera za video wakichana ishara ya vuguvugu la Black Lives Matter katika Kanisa, kuimwagia mafutra ya petroli na kuichoma moto.


Jumapili Mchungaji wa kanisa la Ashbury church alilinganisha kuchomwa kwa bendera hiyo na kuchomwa kwa msalaba.


KWA HABARI, LIVE TV, RADIO, MATOKEO YA LIGI ZOTE DUNIANI DOWNLOAD APP YA M

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad