Akamatwa kwa kumuweka mama yake kwenye jokofu nyumbani kwa miaka 10

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Polisi nchini Japan wamemkamata mwanamke mmoja baada ya mwili wa mama yake kukutwa kwenye jokofu nyumbani kwake.

 

Yumi Yoshino, 48, amesema kuwa alimkuta mama yake akiwa amefariki kisha aliuficha mwili wake miaka 10 iliyopita kwa sababu ” hakutaka kuhama” katika nyumba waliokuwa wakiishi mjini Tokyo, vyombo vya habari vimeripoti, vikinukuu maafisa polisi ambao hawakutajwa majina yao.


Hakukuonekana majeraha yoyote kwenye mwili ulioganda barafu, polisi wameeleza. Mamlaka hawakuweza kuthibitisha muda na sababu ya kifo cha mwanamke huyo. Mwili uliripotiwa kugundulika na mfanya usafi baada ya Bi. Yoshino kulazimishwa kuondoka katika nyumba hiyo kwa sababu ya kukosa kodi.


Mwili ulikuwa umekunjwa kiasi cha kutosha kuingia kwenye jokofu lenye barafu, polisi walisema. Bi Yoshino alikamatwa katika hoteli mjini Chiba karibu na jiji la Tokyo, siku ya Ijumaa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad