Aliko Dangote apoteza mamilioni ya pesa ndani ya siku moja

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mwenyekiti wa kampuni ya Dangote, Alhaji Aliko Dangote, amepoteza kiasi cha dola milioni 900 katika hisa nchini Nigeria, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bloomberg.
Kwa mujibu wa jarida la Bloomberg, ambalo huripoti kuhusu watu 500 tajiri zaidi duniani, mapato ya Dangote yalishuka kwa kiwango cha dola bilioni 18.4 siku ya Alhamisi hadi dola bilioni 17.5 siku ya Ijumaa ,akishuka kutoka mtu wa 106 hadi hadi mtu wa 106 katika orodha ya watu tajiri zaidi duniani , kulingana na gazeti la Punch.

Mwezi Disemba mwaka jana, utajiri wa Dangote ulikuwa na jumla ya thamani ya dola bilioni 17.8 kutoka dola bilioni 15.5 zilizoripotiwa awali.

Dangote alipata mapato ya ziada ya dola milioni 600 katika wiki ya kwanza ya mwezi wa Januari 2021, lakini kapoteza pesa yote hiyo Ijumaa iliyopita.

Hata hivyo Dangote bado ndiye mtu tajiri zaidi barani Afrika na mtu mweusi tajiri zaidi duniani.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad