Donald Trump Afunguka "Imekuwa Heshima Kwangu Kuhudumu taifa la Marekani"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Rais Donald Trump amelihutubia taifa la Marekani kabla hajaondoka madarakani na kusema: "Tumefanya kile ambacho tulikuja kukifanya na tumefanya mambo mengine mengi."

Katika video aliyoiweka kwenye mtandao wa YouTube, alisema "mapambano yalikuwa makali, vita ilikuwa ngumu... kwasababu hicho ndicho mlinichagua kukifanya".


Bwana Trump anaondoka madarakani akiwa bado hakubaliani na matokeo ya uchaguzi wa Novemba, ambao ulimuibua Joe Biden kuwa rais.


Bwana Biden ataapishwa leo Jumatano.


Wiki mbili za mwisho za utawala wa bwana Trump',umekumbwa na ghasia baada ya wafuasi wake kuvamia jengo la bunge la Capitol Hill, wakipinga matokeo ya uchaguzi.


"Ghasia za kisiasa ni shambulio la kila kitu tunachothamini kama Wamarekani. Kamwe hatuwezi kuvumilia," Bwana Trump alisema katika video yake, ambapo bado hakutambua ushindi wa mrithi wake.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad