Fahamu Kiundani Kuhusu Tatizo la Pumu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




PUMU AU ASTHMA NI NINI
Pumu au asthma ni ugonjwa sugu ambao huathiri njia ya hewa ambazo huingiza na kutoa hewa katika mapafu. Ugonjwa huu wa pumu hufanya kuta za ndani ya njia ya hewa kuvimba na hivyo hupunguza kiasi cha hewa kinachoingia na kutoka katika mapafu.

Hali hii husababisha mgonjwa kutoa mlio kama wa filimbi au mluzi wakati wa kupumua pia kubanwa na kifua, kushindwa kupumua vizuri na kukohoa sana,, watu wenye pumu Mara nyingi hupata Dalili hizo wakati wa usiku na asubuhi sana.

Ugonjwa huu huwaathiri watu wa Rika zote ingawaje Mara nyingi huanza utotoni hivyo huwaathiri Zaidi watoto, inasadikika kuwa takribani watoto MILION Sita nchini na watu wazima takriban 255,000 Duniani wanaugua ugonjwa huu.

Ugonjwa huu wa pumu ni mpana sana kwasababu Kuna aina nyingi za pumu kutokana na visababishi vake

AINA ZA PUMU

1. PUMU YA UTOTONI (CHILD_ONSET ASTHMA)

Hii ni aina ya pumu inayotokea baada ya mtoto kuwa Kwenye Vizio kama vile VUMBI LA WADUDU KAMA MENDE, MANYOYA YA WANYAMA KAMA PAKA, MBWA PIA KUTUMIA BABY WIPES ZENYE HARUFU (PERFUME).

Pumu hii hutokea kwa kuwa mwili wa mtoto hutengeneza Kinga ya mwili (ANTIBODIES) zinazosababisha pumu.

Ugonjwa wa pumu ni sugu sana kwa watoto wanaozaliwa na uzito mdogo wenye asili ya kiafrika pia pumu ya utotoni huwaathiri Zaidi watoto wa kiume Zaidi.

(2)PUMU YA UKUBWANI (ADULT_ONSET ASTHMA)

Pumu hii huanza baada ya kufika miaka 20, pumu hii huwaathiri sana wanawake kuliko wanaume na pia haitokei sana kama pumu ya utotoni, Vizio kama vile perfume /cream zenye harufu kali /sabuni nk ndio husababisha pumu hii kwa asilmia kubwa.

(3)PUMU ITOKANAYO NA MAZOEZI (EXERCISE INDUCED ASTHMA)

Pumu hii huwatokea Zaidi wanaofanya mazoezi, ikiwa utakohoa na kukosa pumzi wakati wa mazoezi au baada ya mazoezi kuna uwezekano wa wewe kuwa na pumu ambayo inasababishwa na mazoezi pia hata kama sio mwana mazoezi kukimbia kwa kasi angalau dk 10 Kunaweza kusababisha kukosa pumzi kwa muda mrefu na kuonyesha kwamba una pumu

(4)PUMU ITOKANAYO NA KUKOHOA SANA (COUGH INDUCED ASTHMA

Hii ni aina ya pumu ambayo ni ngumu sana na kuumiza vichwa vya madaktar kuigundua kwasababu katika pumu hii inawezekana isitokee hata Dalili zingine Zaidi ya kukohoa kitu ambacho madaktari wanalazimka kuchunguza sababu nyingine za kukohoa sana na kuhakiksha sio zinasababishwa na kukohoa huko.

(5)PUMU YA USIKU (NOCTURNAL ASTHMA)

Pumu hii hutokea Kati ya saa Sita usiku na saa mbili asubuh, pumu hii huamshwa na vumbi la wadudu rangi ya nyumba, na harufu ya gesi pia Mara nyingi wagonjwa wa pumu hii hushtuka usingizini wakati wa usiku wa manane baada ya kukosa pumzi.

(6)PUMU KALI ISIYOKUBALI DAWA (SEVERE ASTHMA)

Wakati wagonjwa wengi wanapata unafuu baada ya kupata steroid wachache hawapati unafuu na hvyo kuhitaj matibabu makubwa zaid.

(7)PUMU YA NGOZI (ECZEMA /ATOPIC DERMATITIS)

Huenda utashangaa kwamba kuna pumu ya ngozi na ipoje sasa majibu yako yote yamepata majibu, naomba ufahamu kwamba neno ECZEMA ambalo ni neno la kigiriki na linamaanisha KUTUTUMUKA SEHEMU YA NNJE YA NGOZI hali ambayo huonekana pale mtu anapopata maradhi haya.

Ugonjwa huu huchangia asilmia 40 ya maradhi yote ya ngozi kwa ufup huu ugonjwa huwapata Zaidi watoto na tatzo hil limekua likiumiza vichwa vya madaktar na wanasayansi wengi kutokana na kwamba haijajulkana sababu maalum, ugonjwa huu ni wa muda mrefu nikimaanisha kwamba mtu huweza kukaa na ugonjwa huu kwa muda mrefu ingawa si muda wote mwil huonyesha dalil za ugonjwa huu

CHANZO CHA UGONJWA WA PUMU

Visababishi vya pumu havijulkani waziwazi ila vitu vinavyochangia pumu ni vizio mfano Moshi wa sigara, bangi, gesi, perfume, kuwa na msongo wa mawazo, kuogea maji ya moto kila wakati, kutokupaka mafuta, kukaa kwenye vumbi, kuvaa mavazi yasiyo ya pamba,

DALILI ZA PUMU

NOTED :sio watu wote wenye Dalili hizi wanapumu na sio wote wenye pumu Wana

Dalili HIZI

1. Kukohoa~kikohozi huwa kikali wakati wa usiku na asubuhi

2. Kutoa sauti kama mluzi wakati wa kuongea

3. Kubanwa na kifua hasa nyakati za jioni na asubuhi sana

3. Kupungukiwa pumzi

4. Sehemu ya ngozi iliyoathiriwa huwa inatutumka

5. Maeneo yenye atharikubwa yanavimba na kuwa na joto Muwasho wa ngozi huwa mkali wakati wa jioni na usku


Nafasi za Ajira , Jiunge na Group Hili la TELEGRAM Usaidiwe Kutafuta Ajira Bonyeza HAPA Kujiunga


MATIBABU NA JINSI YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA PUMU

Matibabu ya ugonjwa kwa hospital yapo ya aina mbili moja ni Ile ya dharura ili kutoa tu msaada, dawa hii ni zile zinazosaidia kutanua njia ya hewa ambazo zimesinyaa (Bronchopdilators) pia husaidia kulainisha misuli ya njia za hewa iliyosinyaa, aina ya pili ya matibabu ni kutumia dawa za steroid za kuvuta (inhaled corticosteroids)

Ila kwa kawaida matibabu haya huwa chanzo cha matatizo mengine kutokana na kwamba dawa hizo ni za kemikal hivyo huwa si nzur kwani hazimalizi tatizo Zinampa mtu unafuu tu, pamoja na hayo ugonjwa huu unaweza kuzuilika kwa kuepuka kutumia vitu vyenye mzio ambavyo ni PERFUME, SABUNI ZENYE HARUFU KALI, RANGI ZA NYUMBA, KUACHA KUVUTA SIGARA NA BANGI, ACHA KUNYWA POMBE, EPUKA KUVUTA VUMBI LA WANYAMA, NA EPUKA KUKAA MAZINGIRA YENYE UNYEVU.

Ganoderma capsules imetengenezwa kwa viungo vya Spora ganoderma, Cordyceps Sinensis Mycelium, Radix Ginseng


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad