Familia ya Marehemu C Pwaa Waeleza Chanzo cha Kifo Chake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Msanii CPwaa amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo Januari 17, 2021, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, ambako alipelekwa kupata matibabu baada ya kuzidiwa ghafla.


Ndugu yake wa karibu Murad Omary, ameithibitishia East Africa Radio huku akiweka wazi kuwa msanii huyo alikuwa akisumbuliwa na tatizo la Nimonia.


'Cpwaa alilazwa Muhimbili ICU tangu Jumatano ambapo alikuwa anasumbuliwa na tatizo la Nimonia na usiku wa kuamkia leo majira ya saa saba au saa nane hivi tukapigiwa simu kutoka Muhimbili kuwa amefariki'', amesema Murad Omary.


Aidha Murad Omary amesema msiba upo Magomeni kwa mama yake mzazi na CPwaa na mazishi yanafanyika leo saa 10:00 jioni kama hakutakuwa na mabadiliko ya ratiba iliyopangwa baada ya kikao cha familia.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad