Gubu la Wakwe Katika Familia lazua Mauaji ya Mtoto wa Kambi na Wengine Kudumbukizwa Shimoni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Dar es Salaam. Jeshi la Polisi Mkoa linamshikilia Pendo Carlos kwa tuhuma za kumuua mtoto wake wa kambo na kujaribu kuwaua wanaye wawili katika tukio linaloelezwa kuhusishwa na gubu la wakwe zake.


Pendo ambaye kwa sasa yupo mahututi katika Hospitali ya Sinza, Palestina baada ya kujaribu kuondoa uhai wake kwa sumu, anadaiwa kufanya mauaji hayo juzi mchana nyumbani kwake Tegeta A ambapo licha ya kumuua Belinda Carlos (17), pia aliwatumbukiza watoto wake Bertha (4) na Brighton (6) ndani ya shimo la kuvunia maji ya mvua.


Polisi wamethibitisha kutokea kwa tukio na kuwa wanamshikilia mwanamke huyo akiwa hospitalini kwa tuhuma hizo.


Akizungumza na Mwananchi jana, mdogo wake Pendo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema siku ya tukio akiwa katika duka analosimamia alipokea ujumbe kutoka kwa dada yake (Pendo) kuwa anataka kujiua yeye na watoto wake.


“Nilipopata ujumbe huo nilikimbia hadi nyumbani, nilipofika milango ilikuwa imefungwa nikaruka ukuta kuingia ndani, madirisha mengine yaligoma kufunguka, hivyo nikavunja moja kwa shoka,” alieleza.


Soma zaidi gazeti la leo Januari 21, 2021

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad