Jaji: Mwanzilishi wa Wikileaks atajiua akihamishwa hadi Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Mahakama ya Uingereza imekataa ombi la Marekani la kumuhamisha mwanzilishi wa mtandao wa WikiLeaks, Julian Assange hadi Marekani anapokabiliwa na mashtaka ya ujasusi.

Mahakama imeamua kuwa hatua ya kumuhamisha Assange, ni “Ukandamizaji” kutokana na Afya yake ya kiakili.

Jaji Vanessa Baraitser amesema Assange huenda akajiua iwapo atahamishwa hadi Marekani. Hata hivyo, serikali ya Marekani imesema itakata rufaa juu ya uamuzi huo.

Waendesha mashtaka wa Marekani wanamshtumu Assange kwa makosa 17 ya ujasusi na matumizi mabaya ya Kompyuta kwa kuchapisha mtandaoni nyaraka za siri juu ya oparesheni za jeshi la Marekani nchini Iraq na Afghanistan muongo uliopita.

Iwapo atapatikana na hatia, Assange huenda akapewa kifungo cha miaka 175 jela.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad