Kiungo Platinum: Nakuja Simba SC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



NOMORE Chinyerere kiungo kiraka wa FC Platinum ya Zimbabwe amesema kuwa yuko tayari kuja kucheza Simba ambayo inaelezwa imemuwekea dau mezani.

 

Awali chanzo kutoka ndani ya FC Platinum kililiambia Championi Jumamosi kuwa, Simba ilimfuata kiungo huyo mapema baada ya kumaliza mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Taifa wa Zimbabwe ili waweze kupata saini yake baada ya kuvutiwa na uwezo wake.

“Viongozi wa Simba walikuja na kuuliza bei yake kuhusu mchezaji wetu ila kwa kuwa viongozi walikuwa na mchezo wa marudio waliwachunia. Kwa sasa kazi kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika imeisha hivyo ni wakati wa kukaa chini kuzungumzia dili hilo,” kilisema chanzo hicho.

 

Hata hivyo, Championi Jumamosi lilimtafuta Chinyerere ambaye alikuwa kwenye kikosi cha Platinum kilichopoteza kwa kufungwa mabao 4-0 na Simba pale Uwanja wa Mkapa ili aweze kuthibitisha suala hilo ambapo alikiri kufahamu kuhusiana na kuhitajika Simba.“

 

Nimesikia kuhusu kuhitajika ndani ya timu nyingi za hapa Tanzania, nikiwa mchezaji nipo tayari kucheza na ninajua zipo timu nyingi ambazo zinatajwa kuhitaji saini yangu ikiwa ni pamoja na Simba, mimi sioni tabu nitacheza bila mashaka yoyote,” alisema Chinyerere.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad