Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amewatembelea majeruhi wa ajali ya treni katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ambapo ametoa maagizo kwa mkoa kuhakikisha wanasaidiwa kufika makwao mara watakapopata nafuu.
Samia alitoa kauli hiyo baada ya kuzunguka katika wodi zote walikolazwa majeruhi hao na kuzungumza nao lakini akasema ameridhishwa na hali zao pamoja na huduma wanayopata wagonjwa hao.
Kiongozi huyo amefika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma mapema saa moja asubuhi na mbali na kuzungumza na majeruhi wa treni lakini amezungumza na wagonjwa wengine akiwafariji
Msiba mkubwa kwa Taifa.
ReplyDeleteMwenyezi Mungu, Alilaze pema Roho za Marehemu wote na Majeruhi awape Shifaa ya Haraka.
Hii ni Mara ya Tatu hospitali ya Rufaa jijini Dodoma inapokea wagonjwa na Maiti wa Ajali ya treni kwa awamu tofauti. Cha kutaka uangaliwaji ni Eneo limekuwa ni karibia ni Moja.
Tungeomba Hili liangaliwe kwa kina, Hali ya Kijiografia, Tabia nchi ya Eneo husika, Ubora wa Miundo mbinu Athirika.
Na kuuwahusisha Wakazi wa pembezoni mwa Eneo lililosheheni madini asilia yakiwemo Au,Cu, U.
Na milango ya KiuHujumu pia Tuangalie uwezekano wake Kiundani.
Mungu aendelee kutulinda nChi yetu na viongozi wake.