Marekani inasema wavamizi wa bunge walinuia kuwateka na kuwauwa wabunge

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Waendesha mashtaka nchini Marekani sasa wanasema waandamanaji waliolivamia bunge wiki iliyopita walikuwa wanataka "kuwateka na kuwauwa" wabunge. 
Waendesha mashtaka hao wameyasema hayo katika kesi ambayo walikuwa wanamtaka jaji mmoja aendelee kuwazuia Jacob Chansley kutoka Arizona na mtu aliyepigwa picha akiwa amejivalisha pembe akiwa katika afisi ya Makamu wa Rais Mike Pence katika bunge la seneti wakati wa uvamizi huo. 

Mawakili wa idara ya sheria kutoka Arizona walielezea kwa kina kuhusiana na uchunguzi wa idara ya upelelezi Marekani FBI kumhusu Chansley wakisema aliwacha ujumbe kwa Pence akimwambia, ni suala la muda tu kabla haki kupatikana. Chansley anatarajiwa kufikishwa mahakamani baadae leo. 

Idara ya sheria Marekani imewafungulia mashtaka zaidi ya watu 80 kuhusiana na uvamizi huo uliofanyika Jumatano iliyopita.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad