Mke Aamua Kujiua Kisa Mume Kutoka Jela

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Jesca Samson (37) mkazi wa mtaa wa Katoma, Kayanga wilayani Karagwe anadaiwa kujiua kwa kunywa sumu ya panya baada ya kusikia mume wake aliyefungwa kutokana na ugomvi wao ameachiwa kutoka jela.


Mwanamke huyo, kabla ya kifo chake anadaiwa pia alimnywesha sumu hiyo mtoto wake, Jordan Samson (3), ambaye hata hivyo alinusurika kifo.


Kamanda wa Polisi wa Mkao wa Kagera, Revocatus Malimi alisema tukio hilo lilitokea Januari Mosi saa 8:00 usiku baada ya mama huyo kutoka katika mkesha wa Mwaka Mpya 2021.


Jesca, akiwa na ndugu zake, wakitoka kwenye mkesha, alipata taarifa kuwa mume wake ameachiwa huru na baada ya kusikia hivyo, aliwaacha njiani aliokuwa nao na kuwahi nyumbani kisha akanywa sumu hiyo.


Kamanda Malimi alisema baada ya ndugu zake kufika nyumbani, Jesca aliwaambia kuwa amekunywa sumu ya panya, ndipo walimpeleka hospitali ya Wilaya Nyakahanga pamoja na mtoto wake, na mwanamke huyo alifariki dunia Januari 2, huku mtoto wake akipona.


Mumewe ambaye hakutajwa jina, alikuwa amefungwa kifungo cha miezi mitatu jela kutokana na mgogoro wa kifamilia.


“Mgogoro uliokuwapo kati yake na mumewe ulitokana na mwanaume huyo kuuza kipande cha ardhi bila kumshirikisha mkewe na mwanamke akamshtaki katika mahakama ya mwanzo. Mume alihukumiwa kwenda jela miezi mitatu,” alisema Malimi


Alisema baada ya kusikia mme wake ameachiwa kutoka gerezani Desemba 31, 2020 alijenga hofu na hivyo kuchukua hatua za kunywa sumu ya panya na kunywesha mtoto wake.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad