Morrison Ang’ara, Simba Ikiua Wasudan 4-1 Uwanja wa Mkapa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



KIKOSI cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes leo Januari 27, 2021 kimeibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Al Hilal kwenye mchezo wa Simba Super Cup.


Mchezo huo umechezwa Uwanja wa Mkapa na ulishuhudiwa na mashabiki wengi ikiwa ni pamoja na wale waliokuwa wamevaa jezi ya Klabu ya Yanga huku wakionekana kuwa na furaha muda wote.

Ikiwa ni mchezo wa kwanza kwa Gomes ambaye amerithi mikoba ya Sven Vandenbroeck ambaye ametimkia Morocco katika Klabu ya FAR Rabat alishuhudia uwezo wa nyota wake ikiwa ni pamoja na Rarry Bwalya aliyeanza kupachika bao la kwanza dakika ya 39.

Bao hilo lilisawazishwa na Salim Mohamed wa Al Hilal baada ya mabeki wa Simba kufanya uzembe huku Beno Kakolanya akishindwa kuokoa mchomo wa kichwa dakika ya 45.

Kipindi cha pili Perfect Chikwende alipachika bao la pili dakika ya 72 baada ya kipa wa Al Hilal kutema shuti lililopigwa na Bernard Morrison ambaye aliingia kipindi cha pili.


Morrison aliweza kufunga mabao mawili ambapo bao la tatu likiwa ni la pili kwake alifunga dakika ya 86 na lile la pili kwake likiwa la nne kwa Simba alifunga dakika ya 89.

Kocha Gomes amesema kuwa wachezaji wake walipambana kusaka ushindi jambo ambalo limewafanya waweze kuibuka na ushindi huo.


Join Our Telegram Group for Job Updates CLICK HERE


“Wachezaji wamepambana kusaka ushindi na wamefanikiwa hivyo naona kwamba wanastahili pongezi kwa kile ambacho wamekifanya,” .

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad