Mwanamitindo Naomi Campbell atangazwa kuwa balozi wa Kenya wa Utalii

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mwanamitindo Naomi Campbell amekubali uteuzi wa kuwa balozi wa kimataifa wa Utalii Kenya.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Utalii na Wanyamapori, makubaliano hayo yamefikiwa kati ya Campbell na waziri wa utalii na wanyamapori, Najib Balala.

“Tunafurahishwa na taarifa kuwa Naomi Campbell atakuwa balozi wa utalii na kusafiri kimataifa akitangaza Kenya” Waziri amesema.

Wakati wa mkutano huo, Naomi Campbell alisifu serikali ya Kenya kwa kuimarisha miundombinu katika eneo la pwani ikiwa ni pamoja na kuimarisha uwanja wa ndege wa Malindi kuwa wa hadhi ya kimataifa na kuongeza kuwa hatua hiyo itaimarisha utalii katika eneo hilo.

Mwanamitindo huyo maarufu duniani atasaidia kuitangaza Kenya kama eneo ambalo ni kivutio cha utalii duniani.

Bi Campbell amekuwa  akitembelea mara kwa mara eneo la Malindi kuvinjari nyakati za mapumziko yake.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad