Polisi Mbeya wadai dereva wa lori alikuwa na homa ya mapafu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mbeya. Jeshi  la Polisi mkoani Mbeya limesema dereva wa lori, Abrahaman Hussein (61) aliyefariki dunia muda mfupi baada ya kumkamata alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa homa ya mapafu.


Hayo yameelezwa leo Jumamosi Januari 30, 2021 na kaimu kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Jerome Ngowi akibainisha kuwa Hussein  akiwa njiani alijisikia vibaya na madereva wenzake walimpeleka hospitali ya Chimala  na baada ya vipimo alikutwa na ugonjwa huo.


Amesema kwa mujibu wa maelezo ya Peter Kigombola ambaye ni daktari aliyempokea, baada ya kugundua hali hiyo aliwaeleza anapaswa kutengwa na kulazwa.


Amesema kauli ya daktari huyo ilipingwa na madereva waliompeleka Hussein hospitali na walimchukua wakidai atakwenda kutibiwa katika hospitali iliyopo mamlaka ya mji wa Tunduma Mkoa wa Songwe.


Amebainisha kuwa baada ya kutoka hospitali hiyo, Hussein aliendelea kuendesha gari huku akiyumba barabarani na aliyagonga magari mengine na wananchi walitoa taarifa kwa askari wa kikosi cha usalama barabarani kituo cha Inyara wilaya ya Mbeya.


Ngowi amesema baada ya kulizuia gari hilo walimwamuru Hussein kuteremka lakini alikaidi, askari wakalazimika kutumia nguvu kumshusha na kumpeleka kituo cha polisi.




“Kadri muda ulivyokwenda hali yake ilizidi kudhoofu


na hivyo askari waliokuwa zamu wakalazimika kumkimbiza kwenye kituo cha afya cha Igawilo kwa matibabu lakini kwa bahati mbaya alifariki dunia,” amesema


Wakati polisi wakieleza hayo, mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi wa malori Tanzania, Abubakar Msangi ameomba kamati ya uchunguzi iliyoundwa na mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila kukamilisha uchunguzi wake na kutoa taarifa sahihi za chanzo cha kifo cha Hussein.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad