Saido Aanika Alivyoimaliza Simba Sc Akiwa Majeruhi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




SAIDO Ntibanzokiza, kiungo mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa wachezaji wenzake walimuomba awasaidie kuimaliza Simba, Januari 13 licha ya kuwa alikuwa na maumivu jambo ambalo alilifanya kwa kufunga penalti ya ushindi.

 

Ulikuwa ni mchezo wa kwanza kwa Ntibanzokiza ambaye ni ingizo jipya ndani ya Yanga kwenye usajili wa idirisha dogo akiwa ni mchezaji huru kwenye Kombe la Mapinduzi kwa kuwa kwenye mechi tatu hakuwepo kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

 

Yanga ilishinda kwa penalti 4-3 baada ya dakika 90 kukamilika kwa sare ya bila kufungana jambo ambalo limeifanya Yanga kutwaa taji la pili la Kombe la Mapinduzi.

 

Mchezo wa fainali ulichezwa Uwanja wa Amaan ulishuhudiwa na mashabiki wengi waliojitokeza kuona mechi iliyokuwa na ushindani mkubwa.

 

Saido amesema:”Wachezaji wenzangu huwa ninawakubali na wao wananikubali, sasa walipoona mimi nipo na ninaweza kazi wakaniambia twende nami nikafanya kazi.

 

“Mchezo wangu dhidi ya Simba nilicheza licha ya kwamba bado nilikuwa nina maumivu ila nilifanya kwa ajili ya kazi na uwezo wangu mimi ni kucheza.” Yanga inatarajiwa kurejea leo na Kombe la Mapinduzi ambalo wamelitwaa visiwani Zanzibar.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad