AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hatua ya nusu Fainali ya Mashindano ya Kombe la Mapinduzi zitachezwa
leo Jumatatu katika Uwanja wa Amaan kati ya Azam FC vs Yanga Sc
Saa 10:15 jioni na Simba Sc vs Namungo FC saa 2:15 Usiku .
Hayo ni Mashindano ya 15 tangu yalipoanzishwa rasmi mwaka 2007 ambapo
Simba Sc na Mtibwa Sugar zinaongoza kucheza fainali nyingi zikicheza
mara 6 kila timu.
Simba ambayo imecheza fainali 6, tatu ikitwaa Ubingwa na 3 ikipoteza
(2008,2011,2015,2017,2019 na 2020).
Mtibwa Sugar nayo imecheza fainali nyingi (6) za Mashindano hayo ambapo
wameshinda 2 na kupoteza 4 (2007, 2008, 2010, 2015, 2016 na 2020).
Azam ikishika nafasi ya tatu kucheza fainali nyingi za Mashindano hayo
ambapo imecheza fainali 5 na zote imetwaa Ubingwa (2012, 2013, 2017, 2018 na 2019.
Yanga wamecheza fainali 2 wakishinda 1 na kupoteza 1 (2007 na 2011)
sawa sawa na URA ya Uganda ikicheza fainali 2 wakishinda 1 na wakipoteza 1 (2016 na 2018).
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK