Uchaguzi Uganda 2021:Vyama vya upinzani Uganda wameungana kuwa na kituo kimoja cha 'kuhesabia' kura

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Jukwaa linalojulikana kama UID litahusisha matumizi ya teknolojia na nyenzo zingine kuhakikisha kuwa takwimu za matokeo ya uchaguzi kutoka sehemu mbalimbali nchini Uganda yanahakikiwa ipasavyo.
Hii ina maana kuwa wawakilishi wa vyama vyote vya kisiasa kwenye kituo watashirikiana katika kutoa taarifa kuhusu hali ilivyo kuanzia mwanzo hadi mwisho hasa wakifuatilia vitendo ya ukiukaji wa haki za binadamu.

Mwanasiasa mkongwe Paul Semwogerere aliyewahi kuwania kiti cha urais mwaka 1996 dhidi ya rais ndiye mratibu wa jukwaa hilo.

Daktari Kizza Besigye ambaye amewahi kugombea kiti cha urais mara nne na kushindwa na rais Museveni amekanukuliwa kwamba ijapokuwa upinzani ulishindwa kuungana kuwa na mgombea mmoja, muungano huu ni muhimu sana kuweza kukabiliana na jaribio lolote la wizi wa kura.

Vyama vya upinzani nchini Uganda wameungana kuwa na kituo chao kimoja cha kuhesabu kura katika uchaguzi mkuu, vyama hivyo ni NUP, FDC, JEEMA,DP,ANT na mgombea wa kiti cha urais wa kujitegemea Jeneri Henery Tumukunde na Dk.Kiiza Besigye wa serikali ya wananchi.

Mwenyeti wa chama cha Jeema anaelezea kwani wameamuwa kuwa na kituo chao kwasababu tayari chama tawala cha NRM kimetangaza kuwa watakuwa na kituo chao tofauti na tume ya uchaguzi lakini wenye kutangaza matokeo ni tume ya uchaguzi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad