google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Uganda yalaumiwa kwa kuwabana wapinzani | UDAKU SPECIAL

Uganda yalaumiwa kwa kuwabana wapinzani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Shirika la Umoja wa Mataifa la kutetea haki za binadamu limeilaumu mamlaka nchini Uganda na kusema imekuwa ikitumia janga la Covid-19 kama sababu ya kuuzuia upinzani kushiriki kikamilifu kwenye kampeni za uchaguzi wa rais na bunge unaotarajiwa kufanyika wiki ijayo. 
Ofisi ya shirika hilo la kutetea haki za binadamu imesema serikali ya Rais Yoweri Museveni imepunguza idadi ya watu wanaoruhusiwa kuhudhuria mikutano ya kampeni ya vyama vya upinzani kwa kiwango kikubwa na kwamba wagombea wa upinzani na wafuasi wao wanakabiliwa na unyanyasaji, pamoja na kukamatwa kiholela. 

Msemaji wa shirika hilo la Umoja wa Mataifa la kutetea haki za binadamu Ravina Shamdasani aliwaambia waandishi wa habari mjini Geneva kwamba vizuizi hivyo vimewekwa kimakusudi ili kupunguza shughuli za kampeni za uchaguzi kwa upande wa upinzani wakati polisi hawazingatii amri ya vizuizi hivyo katika maeneo ya kampeni za chama tawala.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad