AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wakenya kupitia mtandao wa Twitter wameikosoa wizara ya utalii kwa kumteua mwanamitindo wa Uingereza Naomi Campbell, badala ya kumteua mkenya, kama balozi wa Kenya wa utalii.
Waziri wa utalii Najib Balala katika taarifa yake amesema ilikuwa ni taarifa ya kufurahisha katika sekta hiyo.
Bi Campbell alisifu serikali ya Kenya kwa kuimarisha miundombinu katika eneo la pwani ikiwa ni pamoja na kuimarisha uwanja wa ndege wa Malindi kuwa wa hadhi ya kimataifa na kuongeza kuwa hatua hiyo itaimarisha utalii katika eneo hilo.
Lakini baadhi ya Wakenya wanahisi cheo cha balozi wa utalii kinapaswa kutolewa kwa Mkenya aliyeleta mafanikio kimataifa kama mchezaji filamu Lupita Nyong'o au mchekeshaji Elsa Majimbo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK