Wasaidizi wa rais wa Tunisia waugua baada ya kufungua ‘kifurushi chenye sumu’

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wasaidizi wawili wa rais wa Tunisia wanaugua baada ya kufungua kifurushi kilichofikishwa katika ofisi yao kilichoshukiwa kuwa na sumu , taarifa ya ofisi ya rais imeeleza.

Katika taarifa Mkurugenzi wa ofisi ya rais alikifungua na hakukuta barua yoyote iliyoandikwa ndani ya kifurushi hicho. Hatahivyo baada ya kukifungua ‘’afya yake ilianza kuwa mbaya, na alijihisi kama alikuwa anazimia, alikuwa pia na maumivu makali ya kichwa.


Mfanyakazi mwingine alikuwepo wakati wa tukio, taarifa imeeleza, akapata dalili kama hizo ‘’lakini hali haikuwa mbaya zaidi’’.


Bahasha ilichanwa kablaya kufikishwa kwenye Wizara ya mambo ya ndani, taarifa iliongeza.


Haijulikani ndani ya bahasha hiyo ilikuwa na nini kilichosababisha athari kwa maafisa hao.


Taarifa hiyo imesema vipimo vimechukuliwa na kupelekwa kwenye hospitali ya kijeshi ili kubaini sababu za maafisa kuonesha dalili hizo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad