Waziri wa Ulinzi wa Israel akemea kitendo cha kuwanyima chanjo Wapalestina

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA






Waziri wa Ulinzi wa Israeli Benny Gantz amesema kuwa agizo la kutowapa wafungwa wa Kipalestina katika magereza ya Israel chanjo dhidi ya corona ni uamuzi haramu ambao unahatarisha maisha ya binadamu.


Katika ujumbe wake uliochapishwa kwenye akaunti yake ya Twitter, Gantz alijibu maagizo ya Waziri wa Usalama wa Umma wa Israeli, Amir Ohana, kwamba wafungwa wa Kipalestina katika magereza ya Israeli hawapaswi kupewa chanjo ya Covid-19.



Akisisitiza kuwa maagizo hayo ni kinyume na kanuni ya Wizara ya Afya amesema huo ni uamuzi haramu ambao unahatarisha maisha ya binadamu, Gantz alimtaka Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kuagiza wafungwa wote wenye zaidi ya miaka 60 wapewe chanjo ya Covid-19.



Waziri wa Ulinzi wa Israel amebaini kuwa siasa za vita dhidi ya Covid-19 zingeharibu juhudi za serikali dhidi ya virusi.



Kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya ndani, licha ya kanuni za Wizara ya Afya, Ohana alituma maagizo kwa taasisi husika mwezi uliopita kutowapa chanjo ya Covid-19 kwa wafungwa katika magereza ya Israel.



Katika ripoti hiyo, ilisisitizwa kuwa neno "Wapalestina" halikukutajwa katika maagizo yaliyotumwa na Wizara ya Usalama wa Umma, lakini hakuna wafungwa isipokuwa Wapalestina katika magereza ya Israel.



Kulingana na data ya Chama cha Wafungwa wa Palestina, wafungwa 190 wa Palestina walipatwa na Covid-19 katika magereza ya Israel.



Kulingana na vyanzo rasmi vya Palestina, bado kuna Wapalestina 4,400 katika magereza ya Israel.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad