6 wafariki, 19 watekwa nyara katika Mashambulizi ya silaha Nigeria

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Watu 6 wameripotiwa kupoteza maisha na wengine 19 kutekwa nyara kwenye mashambulizi ya silaha yaliyotekelezwa katika mikoa ya Kaduna na Katsina nchini Nigeria,.
Washambuliaji hao waliokuwa wakiendesha pikipiki waliendesha shambulizi la silaha katika wilaya ya Kajuru iliyoko mkoani Kaduna.

Watu 5 walipoteza maisha katika shambulizi hilo, na wengine 9 wakatekwa nyara huku nyumba nyingi zikichomwa moto.

Katika mkoa wa Katsina, mtu 1 alifariki kwenye shambulizi lililoendeshwa na watu waliojihami kwa silaha, ambapo wanawake 10 pia walitekwa nyara.

Vikosi vya usalama vilitumwa katika maeneo ya tukio na uchunguzi ulianzishwa kuhusu mashambulizi hayo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad