Antonie Nugaz "Tambeni Mtaani Msitembee Kinyonge, Vimbeni Mtaani Kombe Tunachukua"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Afisa Muhamasishaji na msemaji wa klabu ya Yanga SC Antonie Nugaz amewatoa hofu mashabiki wa timu kutokana na matokeo waliyoyapata kwenye mchezo dhidi ya Mbeya City.

Kupitia taarifa aliyoitoa Nugaz amesema ''Mwanachama, mpenzi na shabiki wa Yanga Kwanini ukajikosesha amani kwa timu kutoka sare na kuaminishwa Kuwa timu haitopata matokeo na wewe unaamini hilo.


Kumbuka mpaka sasa tuko kileleni (Namba moja) kwenye msimamo wa ligi na pia tukiwa na rekodi sahihi ya kutopoteza Mchezo hata mmoja.


Lazima tukubaliane na matokeo ya Mpira na sio kulaumu sana kana kwamba tuko nafasi ya 8 au tunaburuza mkia.


Tambeni Mtaani msitembee kinyonge,vimbeni mtaani na muendelee kuipa hamasa timu yetu Insha Allah kila kitu kitaenda Sawa.


Kisha tukutane Uwanja wa Benjamin Mkapa siku ya jumatano kwenye Mchezo wetu dhidi ya Kagera Sugar saa 1 Kamili usiku Tujitokeze kwa wingi bila kukosa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad