Azam FC kuvaana na TP Mazembe kesho

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



KLABU ya Azam FC inayonolewa na Kocha Mkuu, George Lwandamina kesho itakuwa na kazi ya kusaka ushindi kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Klabu ya TP Mazembe.

Januari 30, Azam FC ilishinda mabao 3-1 dhidi ya KMC kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Azam Complex majira ya saa 10 jioni.


Mabao ya Azam FC mawili yalifungwa na nyota wao Prince Dube na moja lilifungwa na Mudathiri Yahaya huku lile la KMC likifungwa na Lusajo Mwaikenda.


Kesho Februari 2 Azam FC inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya miamba ya Afrika, TP Mazembe ambao ni washindi wa tatu wa mashindano ya Simba Super Cup.


Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema kuwa malengo ya mchezo huo ni kuendelea kujiweka sawa kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu Bara.


Azam FC ikiwa nafasi ya tatu kwenye msimamo inatarajiwa kucheza Februari 7 na Simba ambao ni mabingwa wa Simba Super Cup, Uwanja wa Mkapa.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad