Bobi Wine Aifuta Kesi Dhidi ya Museveni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




KIONGOZI wa chama cha upinzani nchini Uganda cha National Unity Platform (NUP), Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine ameondoa mashtaka yake ya kupinga uchaguzi wa urais wa Uganda aliyowasilisha dhidi ya Rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni.

 

 

Alitaja hatua ya jaji kukataa kuongezea ushahidi zaidi uliowasilishwa na timu yake kama sababu ya kuondoa kesi hiyo.

 

 

Pia, ameongezea kuwa suala hilo litaamuliwa na wananchi lakini akatoa wito kwa wafuasi wake kutojihusisha na ghasia.

 

 

Hatua ya Bobi Wine inakuja siku moja baada ya Rais Museveni, Tume ya Uchaguzi na Mwanasheria Mkuu kuwasilisha hati zao za kiapo 185 kujibu sababu 53 ambazo timu ya wanasheria ya NUP ilikuwa imeibua kuthibitisha kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa wizi, na haukuwa huru na wa haki.

 

 

Chama cha Rais Museveni pia kimetuma ujumbe wa Twitter kuwa Museveni amepata ushindi katika kesi hiyo.

 

 

Siku ya Jumapili, mawakili wa chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) walisema Bobi Wine atakabiliwa na athari kubwa za kifedha ikiwa atathubutu kuondoa ombi la kupinga ushindi wa Museveni kwenye Mahakama Kuu.

 


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad