Dereva aliyekimbia ajali iliyosababisha kifo cha Kwitega asakwa na polisi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Dereva wa basi la kampuni ya Makara lililogongana uso kwa uso na gari la aliyekuwa katibu tawala Mkoa wa Arusha, Richard Kwitega anatafutwa na polisi baada ya kutoroka.


Katika ajali hiyo iliyotokea jana, Kwitega alifariki dunia huku watu wanne wakijeruhiwa ambao ni dereva wa Kwitega na wanawake watatu waliokuwa katika basi hilo.



Akizungumza na Mwananchi Digital leo Alhamisi Februari 4, 2021 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Harrison Mwakyoma amesema wanamtafuta dereva huyo aliyetoroka baada ya kutokea kwa ajali hiyo.



"Dereva aliyekuwa anaendesha gari la katibu tawala, Constantine Lubango yupo hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Manyara mjini Babati akiendelea na matibabu ila bado tunamtafuta aliyekuwa anaendesha basi la Makara," amesema Mwakyoma.



Amesema bado hawajabaini  chanzo cha ajali hiyo, “tutatoa taarifa kamili ya chanzo cha ajali hiyo mara baada ya uchunguzi wa polisi kukamilika.”



Kwa mujibu wa mganga wa hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Manyara, Dk Yesige Mtajwa majeruhi wa ajali hiyo wanaendelea vizuri.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad