Ishu ya Ndayiragije Kuchimbishwa Taifa STARS Ngoma Nzito

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

  


 IKIWA tetesi zinaeleza kuwa Ettiene Ndayiragije, Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzana, Taifa Stars amesitisha mkataba wake, Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) limesema kuwa lina utaratibu maalumu wa kutoa taarifa.

Ndayiragije alishindwa kukiongoza kikosi cha Stars nchini Cameroon kutinga hatua ya robo fainali kwenye mashindano ya Chan ambayo yanawahusu wachezaji wa ndani nchini Cameroon.


Kutokana na kuboronga huko inaelezwa kuwa amechimbishwa ndani ya Stars ili kuweza kumpata kocha mpya ambaye atakuwa ndani ya Stars.


Stars ilikusanya pointi nne baada ya kucheza mechi tatu, ilishinda moja, sare moja na ilichapwa mechi moja ya ufunguzi kwa mabao 2-0.


Kombe la Chan limekwenda tena nchini Morocco ambao walikuwa ni mabingwa watetezi wa taji hilo ambalo walilitwaa 2018 na kulifanya taifa hilo kutwaa taji hilo mara mbili.


 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad