Jela miaka 30 kwa kumlawiti mtoto wa miaka 15

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Serengeti imemhukumu Mageta Masaro (29) mkazi wa Nyakitono kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kumlawiti mtoto wa miaka 15.



Hakimu mkazi mfawidhi wa Wilaya Serengeti,  Ismael Ngaile katika kesi ya jinai namba  117/2020 leo Ijumaa Februari 26, 2021 amesema ushahidi wa watu sita uliowasilishwa na Serikali haukuacha shaka.




Amesema kutokana na kukithiri kwa matukio ya ubakaji mahakama inalazimika kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wengine.




Mwendesha mashtaka wa Serikali, Renatus Zakeo amesema Aprili 24, 2020 mshtakiwa alimtumia binti aliyekuwa akiishi nyumbani kwao kumuita mtoto huyo mwanafunzi wa shule ya msingi Nyakitono na alipofika alimkamata na kumlawiti.




Amesema mtoto huyo alipiga kelele na wananchi wakajitokeza na kumkamata mshtakiwa, na mtoto huyo alipopimwa iligundulika kuwa amelawitiwa.




Alibainisha kuwa hawana rekodi ya matukio ya mshtakiwa lakini ameiomba mahakama itoe adhabu kulingana na kosa alilokuwa nalo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad