Jeshi la Yemen latangaza kumuua kamanda wa Houthis na wanamgambo kadhaa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jeshi la Yemen limetangaza kumuua kamanda mmoja wa Houthis pamoja na watu wengine kadhaa wanaohusika na vikosi hivyo vya kijeshi katika eneo la Hudayda Magharibi mwa nchi.

Katika maelezo yaliyotolewa na makamanda wa Amalika wa jeshi la Yemen, iliarifiwa kuwa mashambulizi ya wanamgambo wa Houthis yalitibuliwa na kuzuiwa na jeshi katika eneo la “Kilo 19” Mashariki mwa Hudayda.


Kamanda wa Houthis Ibrahim Al-Deylemi pamoja na wanamgambo kadhaa waliuawa walipokuwa wakitaka kuingia kwenye ngome za mawasiliano katika eneo hilo.


Kundi la Houthis halijatoa taarifa yoyote kuhusiana na tukio hilo.


Serikali na viongozi wa Houthis walikutana mjini Stockholm nchini Usiwidi Desemba 2018 kwa ajili ya mazungumzo ya kumaliza mzozo na kutia saini makubaliano ingawa bado kumekuwa na mvutano katika eneo la Hudayda kutokana na tuhuma zinazoendelea kati ya pande zote.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad