Kasi ya Simba Yampa Presha Cedric Kaze Yanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





KOCHA Mkuu wa Yanga, Mrundi, Cedric Kaze amefi chua kuwa kwa sasa wamekuwa kwenye presha kubwa ya kuhakikisha wanapata matokeo katika kila mchezo kutokana na kasi ya wapinzani wao wakiwemo Simba kuelekea kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu.

 

Kaze ametoa kauli hiyo ikiwa Yanga inaongoza ligi kwa pointi 49, ikifuatiwa na Simba wenye pointi 42 huku wakifuatiwa na Azam wakiwa na pointi 36.

Akizungumza na Championi Jumatano,Kaze alisema kuwa matokeo wanayopata kwa sasa yamekuwa yakiongeza presha kwao lakini wataendelea kupambana kwa kuhakikisha wanafi kia malengo.



“Hatujawa kwenye kipindi kizuri kwa sasa hasa upande wa matokeo, presha imekuwa kubwa upande wetu kwa sababu kila aliyekuwa nje anataka kuona matokeo mazuri na hilo ndiyo lengo letu kuona tunafanya hivyo.

 

“Kikubwa tunachokiangalia ni malengo ya timu kuweza kufi kiwa kwa pamoja na kuweza kuondoa presha ambayo tumekuwa nayo kwa sasa kutokana na matokeo ya mechi ambazo zimepita na kasi kubwa ambayo wamekuwa nayo wapinzani (Simba), wetu ambao wamekuwa wakishinda michezo yao mfululizo,” alisema Kaze.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad