Kenya yawazuia wanariadha wake kushiriki Kimanjaro Marathon

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Kenya imekataa kuwaidhinisha wanariadha wake kushiriki mbio za masafa marefu za Kilimanjaro Marathon nchini Tanzania kwa kuhofia janga la corona.
Mashindano hayo yanayotambuliwa na Shirikisho la Riadha Duniani IAAF- yataandaliwa e Jumapili hii chini ya mlima Kilimanjaro, mlima mrefu zaidi barani Afrika.

Wanariadha wa Kenya wamekuwa wakitawala mbio hizo katika makala yaliopita.

Katika taarifa, Shirikisho la Riadha la Kenya limetoa wito kwa "wanariadha wote kutosafiri Tanzania kushiriki mashindano hayo".

Tanzania haijakuwa ikitoa data ya hali ya corona nchini humo tangu kati kati ya mwaka jana.

Mapema wiki hii Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitoa wito kwa Tanzania kuanza kutoa data ya watu walioambukizwa virusi vya corona.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad