Kim alalamika kuhusu hali mbaya ya kiuchumi Korea Kaskazini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amelaumu baraza la mawaziri kwa kutofaulu kwa mpango wa miaka 5 wa maendeleo uliowekwa mnamo 2016.
Kulingana na ripoti ya Shirika la Habari la Korea Kaskazini (KCKN), Kim alilalamika kuwa baraza la mawaziri halikuweza kutimiza jukumu lake kama "taasisi muhimu inayosimamia uchumi" na kwamba ilikuwa ikitoa mipango isiyofaa bila "mtazamo wa ubunifu na mbinu wazi" .

Kim amesema kuwa kutokana na vifaa vichache vya kilimo na hali mbaya, malengo ya uzalishaji wa kilimo wa baraza la mawaziri kwa mwaka huu yamewekwa juu sana.

Akisisitiza kuwa lengo lililowekwa la uzalishaji wa umeme ni la chini sana, Kim alibainisha kuwa uhaba ambao unaweza kutokea unaweza kusimamisha kazi katika migodi ya makaa ya mawe na viwanda vingine.

Kim amesema kuwa baraza la mawaziri halikuchukua jukumu la kuongoza katika kubainisha mipango ya maeneo muhimu ya uchumi.

Akiongea kwenye Kongamano la Chama cha Wafanyakazi la Korea lililofanyika Januari 6, baada ya mapumziko ya miaka 5 katika mji mkuu wa Pyongyang, Kim alikiri kwamba karibu sekta zote za nchi hiyo zilibaki nyuma ya mipango yao ya maendeleo ya uchumi, na kwamba mpango wa maendeleo wa miaka 5 uliowekwa mnamo 2016 umefeli.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad