Madaktari wasifu kufanikiwa kwa upandikizaji wa kwanza wa uso na mikono

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA






Joe DiMeo, 22, alifanyiwa upasuaji huo wa saa 23, uliofanywa na timu ya zaidi ya wahudumu wa afya 140 mwezi Agosti mwaka jana.


Ajali ya gari mwaka 2018 ilimwacha Bw DiMeo na majeraha ya kuungua kwa kiwango cha zaidi ya 80% ya mwili wake. Vidole vyake vilikatwa na alipoteza midomo na vigubiko vya macho.



Alisema operesheni hiyo ilimpa "nafasi ya pili maishani".



Bwana DiMeo alikuwa akienda nyumbani kutoka zamu ya usiku alipolala kwenye usukani. Gari lake lilianguka, likawaka moto.



Alikaa miezi minne katika kitengo kinachoshughulika na wagonjwa walioungua moto, ambacho kilijumuisha wakati alipokuwa hana fahamu . Kisha Bwana DiMeo alikuwa na upasuaji zaidi ya mara 20 wa kutengeneza mwili.



Mwaka 2019, alipelekwa kwenye kituo cha matibabu cha kitaaluma huko New York, NYU Langone, ambapo alifanyiwa upasuaji wa upandikizaji mwezi Agosti mwaka jana.



Eduardo Rodriguez, mkurugenzi wa Programu ya Kupandikiza Uso, alisema: "Tulitaka kumpa sio tu operesheni ambayo ilimfanya aonekane bora, lakini mwishowe ilibidi ifanye kazi vizuri, hasa mikono."



Bwana DiMeo alitumia siku 45 akiwa chini ya uangalizi baada ya upasuaji na miezi miwili zaidi hospitalini, ambapo alilazimika kujifunza jinsi ya kufungua vigubiko vya macho na kutumia mikono yake mipya.



Upandikizaji wa uso na mikono miwili uliwahi kufanyika hapo awali lakini yote haikufanikiwa. Mgonjwa mmoja alikufa kutokana na changamoto na mwingine mikono yake iliondolewa baada ya kushindwa kufanya kazi, hospitali ilisema.



Bw Rodriguez anasema Bw DiMeo, ambaye hufanya hadi saa tano za ukarabati kwa siku, ndiye "mgonjwa aliye na motisha zaidi" aliyewahi kukutana naye.



"Anataka kufanya kazi kwenye michezo, anapenda kucheza gofu, na anataka kurudi kwenye kozi. Ninavutiwa kila wakati na kiwango cha uzani ambao anaweza kuinua

 DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL HAPA KUPATA HIZI HABARI KWENYE SIMU YAKO HATA BILA BUNDLE


Bwana DiMeo anasema sasa anaweza kufanya mazoezi mwenyewe na kutengeneza kifungua kinywa.



"Hii ni zawadi ya mara moja katika maisha, na natumaini familia inaweza kupata faraja kujua kuwa sehemu ya wafadhili inaishi na mimi," alisema. "Wazazi wangu na mimi tunashukuru sana kwamba nimepewa nafasi hii ya pili."


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad