Mbunge amwagiza Polepole awapelekee CCM ujumbe huu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mbunge wa Konde kupitia Chama cha ACT Wazalendo Khatib Haji, amemwagiza Mbunge wa kuteuliwa Humphrey Polepole, aende akawaambie wana CCM ambao bado wanataka Rais Dkt. Magufuli, aongeze muda wa madarakani kwamba alikwishasema hawezi kuongeza muda hivyo wasimlazimishe.


Kauli hiyo ameitoa hii leo Februari 9, 2021, Bungeni Dodoma, wakati akitoa pongezi kwa Rais Dkt. Magufuli, kwa kuamua kuiheshimu na kuilinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo licha ya wanachama wenzake kutaka asiondoke madarakani lakini yeye amekwishaweka msimamo wake siku nyingi kwamba akimaliza wamu zake ataondoka.


"Magufuli atakuwa ni Rais wa kwanza kwa nchi za Afrika ambaye baadhi ya wabunge wake wanamuomba aongeze muda lakini tayari ameweka msimamo. Polepole waambie CCM Rais hana shida ya kuongeza muda alikutuma na video zinatembea tunaziona kwanini unawaacha akina Sanga hapa wanaendelea kupotosha?, kwanini hamuheshimu mawazo ya Mh. Rais?", amesema Mbunge Khatibu.


Akijibu hoja hiyo Polepole amesema kuwa, "Mimi naomba nitumie nafasi hii kumpa taarifa Mbunge, kwamba masuala ya CCM yanzungumziwa kwenye vikao vya chama hapa Bungeni, wabunge wana uhuru wa kutumia uhuru wa Bunge kuzungumza lakini kinachozungumzwa hapa ndani hakiathiri msimamo wa chama tumekwishautoa Rais hataongeza muda".

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad