Morrison, Mugalu Gumzo Kila Kona Kinshasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MASHABIKI wa soka jijini hapa wanazungumzia zaidi uwepo wa Bernard Morrison na Chris Mugalu kwenye kikosi cha Simba kitakachowavaa AS Vita Ijumaa saa 3 usiku.


Simba imetua Kinshasa na wachezaji 27 ili kujiweka tayari kwa lolote linaloweza kutokea hata kama baadhi yao watakumbana na mizengwe ya ugonjwa wowote.


Kwa mujibu wa mchambuzi na mtangazaji mahiri wa michezo kwenye redio maarufu ya Top Congo FM, Jenovic Mbowa wachezaji hao wawili ndio wanaosemwa sana na wanapewa nafasi kubwa ya kusumbua kwa vile wanaielewa vizuri DR Congo na aina ya soka na mambo ya ndani na nje ya uwanja.


Alisema Morrison kama akiongeza umakini kwenye kufunga ndiye anayeweza kuwa na madhara zaidi ndani katika mechi hiyo kwa vile wanamjua.


“Mugalu ni mchezaji mzuri na isitoshe ni Mkongo, anaelewa mambo mengi ya hapa kwa vile alicheza sana FC Lupopo ya Lubumbashi anawajua sana Vita, atasumbua,” alisema



-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad