Mshirika wa Muimbaji R Kelly Ashikwa Akitaka Kumuhonga Shahidi Bilioni Moja ili Asitoe Ushahidi Dhidi ya R Kelly

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


 Richard Arline Jr. ambae ni mmoja wa Washirika wa R.Kelly amepatikana na hatia ya kujaribu kumhonga Mwanamke mmoja ili asitoe ushahidi dhidi ya R.Kelly Mahakamani.


Inaaminika Mwanamke huyo ni miongoni mwa Wanawake ambao R.Kelly alishiriki nao mapenzi kabla ya umri sahihi na ana siri nyingi za Mwimbaji huyo ambapo kwenye sauti za ushahidi zilizopatikana, Richard alisikika akimwambia Mwanamke huyo kwamba atampatia $500,000 (Tsh. Bilioni 1.1) ili akatae kwenda kutoa ushahidi Mahakamani dhidi ya R.Kelly.


Richard ni miongoni mwa Wanaume watatu ambao wameshitakiwa kwa kujaribu kuharibu ushahidi wa Mashahidi dhidi ya kesi ya R.Kelly ambapo June 2021 hukumu ya Richard itatolewa na kifungo cha kosa kama lake kinaweza kufikia hadi miaka 15 jela.

 DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL HAPA KUPATA HI
ZI HABARI KWENYE SIMU YAKO HATA BILA BUNDLE

R.Kelly (54) amekua akishikiliwa gerezani na kunyimwa dhamana wakati akisubiri kusikilizwa kwa kesi yake akidaiwa kuongoza kundi la Uhalifu kwa muda mrefu kusajili Wanawake na Wasichana na kufanya nao mapenzi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad