Rayvanny; Nitaondoka WASAFI (WCB) kwa amani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Msanii Raymond Shaban Mwakyusa AKA Rayvanny aliyepo chini ya label ya Wasafi Classic Baby (WCB) amesema atahakikisha anatoka kwenye label hiyo kwa amani. Katika kipindi cha Salama Na Rayvanny kinachorushwa EATV aliulizwa na Salama kuwa wapo watu wanasema Rayvanny ndiye anayefuata kuondoka WCB baada ya Harmonize, Rayvanny alisema jambo hilo linawezekana, na wanaosema hayo wanaongea kwa kuwa yeye ni msanii anayefanya vizuri WCB. Rayvanny alisema Kama ukifika wakati wa yeye kuondoka WCB basi atahakikisha anaondoka kwa amani bila migogoro yoyote.

NINA TABIA NJEMA

Katika mambo mengine aliyosema Rayvanny ni kwamba yeye hanywi pombe, havuti sigara wala bangi hata hivyo alikataa kutaja starehe anayoipenda. Amedai yeye ni mtu anayemtegemea na kumwamini Mungu na kwamba mama yake ni mlokole wa dhehebu la Baptist huko mkoani Mbeya ambapo pia amedai yeye alikuwa akiimba kwaya kanisani.

Anasema hajawahi kwenda kwa mganga na haamini katika kutegemea nguvu za giza.

MSISHANGAE SIKU NIKIIMBA GOSPEL

Katika kuthibitisha ucha Mungu Rayvanny amesema watu wasijekushangaa siku akiacha bongo flavor na kuhamia kwenye muziki wa injili.

SIPO SINGLE

Pamoja na kukataa kumtaja anayedate naye Rayvanny amesema kwa sasa hayupo single.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad