AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Katibu Mkuu Wizara ya Afya nchini Tanzania, Profesa Mabula Mchembe amesema hospitali hazijajaa wagonjwa wenye shida ya mfumo wa hewa kama inavyoelezwa, akibainisha wengi wapo katika wodi za upasuaji.
Profesa Mchembe ameyasema hayo leo Jumamosi Februari 13, 2021 alipofanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC) pamoja na kuangalia mwenendo wa utoaji wa huduma za afya katika hospitali hiyo.
"Wafanyakazi wanaohudumia wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa hewa wana afya njema wala hawajapata matatizo. Ukiangalia hospitali sio kama wanavyosema kwamba zimejaa wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa hewa, hapa nimekuta wagonjwa wengi zaidi katika wodi za upasuaji," amesema Profesa Mchembe.
Amebainisha kuwa kwa sasa wataongeza nguvu katika upande wa upasuaji ili wananchi wasikae hospitali kwa muda mrefu.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK