Uwoya Atamba Bado Ana Muda Kula Ujana 'Ndoa zinavunjika Kila Siku Kwanini Niingie Huko'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




LICHA ya kwamba ni mama mwenye mtoto mkubwa tu, Krish Ndikumana, staa wa Bongo Movies, Irene Uwoya, eti ametamba kwamba, bado ana muda mrefu wa kuendelea kula ujana wake vizuri bila kuwa na mwanaume yeyote wa kuishi naye ndani mpaka atakapoona ametosheka vilivyo ndipo atakapofikiria kuolewa.





Akizungumza na Gazeti la IJUMAA, Uwoya au Mama Krish anasema kuwa, kuna wakati mwingine baadhi ya wanawake wanakuwa hawajamaliza kula ujana vizuri hivyo wakiingia kwenye ndoa hawakai na mwisho wa siku ndoa inavunjika.


“Wanawake wengi wanakimbilia kwenye ndoa mapema, lakini baada ya muda ndoa inavunjika maana bado wanatamani sana mambo ya nje na hata mimi nimejifunza hivyo kwa sasa nakula kwanza ujana mpaka nitosheke, halafu nikishaingia kwenye ndoa, nitakaa kwa kutulia,” anasema Uwoya mwenye umbo matata.

Stori: Khadija Bakari, Dar
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad