FIFA yalia kifo cha Rais Magufuli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Jumuiya ya soka kimataifa 'FIFA' limetuma salama za rambi rambi kwa shirikisho la soka nchini TFF kufuatia kifo cha Rais, Hayati, Dk.John Pombe Magufuli kilichoripotiwa kutokea siku ya Jumanne tarehe 17 Machi 2021 kwenye Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam kutokana na maradhi ya moyo.


Kwa niaba ya wajumbe wa jumuiya ya soka kimataifa, Rais wa jumuiya hiyo Gianni Infatino ameandika kuwa:


“Ilikuwa hisia ya huzuni kupata taarifa za kifo cha Rais Dk.John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.”


“Tunapenda kuungana na wote wanaotoa salam za pole kutoka pande zote Duniani.”


“Akiongoza toka mwaka 2015, kiongozi mwenye haiba ya juu, aliyetambulika kwa maono yake, uzalendo, matendo ya Utawala bora na kupiga vita rushwa na umasikini, Rais, Dk.John Pombe Magufuli hatosahaulika”.


“Kwa niaba ya wajumbe wa jumuiya ya soka kimataifa, tunapenda kutoa pole kwa shrikisho la soka nchini Tanzania 'TFF', serikali na watanzania kwenye kipindi hiki kigumu”.

 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad