Hatuoni tabu kuomba radhi kama tulitofautiana huko nyuma –Mwenyekiti UVCCM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM Taifa (UVCCM) Kheri James amesema UVCCM haioni tabu kuomba radhi kwa yeyote iwapo kuna mambo waliyafanya huko nyuma ambayo yalichochea chuki na uhasama na kuteteresha umoja na mshikamano wa Watanzania.
“Yawezekana katika siasa zetu na hekaheka zetu tuliweza kutofautiana kimitazamo, yapo mambo ambayo huko nyuma yalipelekea umoja wetu ukaterereka, UVCCM hatuoni aibu kusema tunaomba radhi kwa hayo kama tuliyatenda na tupo tayari kurekebisha ili kutengeneza jukwaa safi kwa Rais wetu kuanza upya akiwa na Watu walioshikamana na kuwa wamoja ili Nchi yetu iweze kwenda mbele”

“Sisi kama Vijana wa Mapinduzi kote Nchini tunao wajibu wa kushirikiana na Vijana wenzetu kuilinda dhamira hii ya Rais wetu ya kuwaleta Watanzania pamoja, kujenga mshikamano wao, kuzika tofauti zetu, ya kufungua kurasa mpya utakaotoa dira ya usawa, haki na maendeleo ya ukweli kwa Watanzania wote”

“Sisi Umoja wa Vijana CCM kamwe hatutokuwa kikwazo cha dhamira hiyo, kama kuna jambo huko nyuma ambalo kwa maneno au matendo ambalo linaweza kutumika kama rejea ya kuzuia hiyo dhamira ya Rais wetu sisi tunasema tunaomba radhi na tuko tayari kushirikiana na Rais wetu ili kuhakikisha dhamira yake haikwamishwi na matendo wala maneno yetu” – Kheri James.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad